Abdallah Saleh

Mchambuzi
Mchambuzi wa habari za mpira wa miguu katika kituo Times FM.
Ligi Kuu

Chirwa anahitaji Msaada

Sina tatizo na Tff wala kamati zake na hata muda uliotumika kupitia vielelezo pia naona ulikuwa sahihi kabisa kutokana na uhalisia wa jambo lenyewe Ndio ilikuwa sahihi kwa maana Obrey Chirwa aliitwa na Tff, lakini alikuwa kwao Zambia akifanya shughuri zake za kilimo na hata aliporudi nchini aliunganisha Zanzibar kwenye...
EPL

United yaibanjua Stoke City

Manchester United imepata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Stoke City, katika mchezo wa ligi kuu ya soka Uingereza maarufu kama EPL Katika mchezo huo uliofanyika usiku wa kuamkia leo kunako dimba Old Trafford, Manchester United walipata bao la uongozi mapema dakika ya 9 kupitia kwa Antonio Valencia akimalizia kazi...
Ligi Kuu

Masoud Djouma amkaribisha Okwi

Kocha wa Simba sc Masoud Djouma, amezungumza na mchezaji wake Emmanuel Arnold Okwi na huenda leo asubuhi akaanza mazoezi na wenzake Kiungo mshambuliaji huyo ameungana na kambi ya Simba iliyopo Morogoro, wakijiandaa na mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara dhidi ya Singida United Okwi aliyewasili nchini leo akitokea...
EPL

Tathmini ya mchezo uliopoteza rekodi ya Man City

Hakika ilikuwa ni vita kati ya 'Gegenpressing' ya Jugen Klop dhidi ya 'Tik tak' ya Pep Guardiola, pamoja na kuonekana kama ni aina ya uchezaji unaofanana lakini kuna utofauti mkubwa wa 'patterns' za uchezaji ndani ya kiwanja huku zote umiliki wa mpira ukiwa ndio msingi mkuu Klop anayetamba na Gegenpressing...
Mapinduzi Cup

Azam fc yatetea ubingwa wake

Klabu ya Azam fc imefanikiwa kutetea ubingwa wake wa kombe la mapinduzi, baada ya kuilaza URA kwa penati 4-3 kufuatia matokeo ya sare ya 0-0 katika dakika 90 za kawaida Katika mchezo huo ulioamuliwa na mwamuzi Mfaume Nassor aliyesaidiwa na Mbaraka Haule na Dalila Jaffary, ukihudhuliwa na Rais wa Zanzibar...
Ligi Kuu

Mbeya City FC yafanya mabadiliko

Klabu ya Mbeya city fc, imefanya mabadiliko katika benchi lake la ufundi kutokana na uhitaji na nafasi; mabadiliko haya yanahusisha nafasi ya Kocha Msaidizi, Meneja wa Timu na Mtunza vifaa. Mwalimu Mohamed Kijuso amerejea katika timu yake ya awali (Timu B) na ataendelea kuwa kocha wa timu hiyo yenye nyota...
Uhamisho

Pep anavyomuhitaji Sanchez

Kwanza tunaanza kumtazama Pep Guardiola namna alivyokijenga kikosi cha Manchester city aina ya uchezaji kwenye kikosi chake. Pep ni moja kati ya walimu wajanja sana, ukiangalia kikosi cha Manchester city namna kinavyocheza licha ya kumsukuma mpinzani kurudi kwenye eneo lake, lakini pia imekuwa na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira kwenye...
La Liga

Haya ni mambo 10 usiyoyajua kuhusu Pepe

Anaitwa Levran Lima Pereira maarufu kama Pepe Alizaliwa na kukulia chini Brazil lakini alitimkia Ureno akiwa na umri wa miaka 18 Mwaka 2006, baba yake mzazi alisema kuwa amepigiwa simu na kocha wa timu ya taifa ya Brazil akimuhitaji Pepe kikosini lakini mchezaji huyo alikataa na kuamua kuichezea Ureno Alipojiunga...
Uhamisho

City wamkomalia Sanchez

Klabu ya Manchester city wanataraji kutoa ofa mpya kwa mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez 29, na wanaamini kuwa Arsenal wataruhusu raia huyo wa Chile kuondoka mwezi huu Sanchez yuko tayari kurejea kima cha pauni milioni 25 kuhakikisha kuwa anajiunga na Manchester city Arsenal watamruhusu Sanchez kuondoka endapo watapokea hadi pauni...
1 14 15 16 17
Page 16 of 17