Galacha wa Hat-Trick

Galacha wa Hat-Trick, ni kipengele ambacho kitawatambua wachezaji ambao wanafunga magoli matatu  katika mchezo wa ushindani katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.

Lengo ya kipengele hiki ni kuendelea kutoa chachu kwa washambuliaji kufunga mabao mengi zaidi katika mechi zao.

Katika Msimu huu wa 2019/2020 mtandao wetu unaendelea kurekodi Hat-Trick zote na mwisho wa msimu tutaangalia mchezaji gani ana Hat-Trick nyingi zaidi ili aweze kupewa zawadi. Iwapo wachezaji watafungamana, basi tutaangalia katika mchezo husika mchezaji huyo kama alikuwa na ziada ya zaidi ya goli moja au hat-trick pacha.