Blog

Tanzania kupeleka timu nne kwenye michuano ya CAF ?

Sambaza....

Zimebaki asilimia 10 tu kwa Libya kuipiku Tanzania nafasi 4 za uwakilishi michuano ya vilabu CAF.Matokeo ya jana Kati ya Ac Djoliba toka Mali dhidi ya Al Nasr Bhengazi toka Libya kwa Ac Djoliba kukubali kichapo Nyumbani 0-1 yameiweka Al Nasr kwenye nafasi Bora kufuzu hatua ya robo fainali michuano ya shirikisho.

Al Nasr Sasa Wana point 8 nyuma ya Horoya Ac ya Guinea yenye point 10 ambayo tayari imeshafuzu,Ac Djoliba ni watatu Wana point Tano, mechi za mwisho katika hatua ya makundi zitachezwa Jpili ya tarehe 2 ambapo Al Nasry atakua Nyumbani kuwakaribisha Horoya Ac na Ac Djoliba watakua ugenini South Africa kukabiliana na Bidvest Witts .

Al Nasr wanahitaji sare tu ama hata wakifungwa na ac Djoliba wakatoka sare na Bidvest Basi Al Nasr ataungana na Horoya ac Kwenda hatua ya robo fainali kitendo kitakachongeza point za Libya kufika 16.5 na kuiacha Tz na point 14… Kiufupi mwakani tz wawakilishi wawili Bingwa VPL -Klabu bingwa Africa,ingwa Azam Sport Federation Cup-Kombe la Shirikisho.

Sambaza....