Lakini pia ndio timu pekee kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) iliyofika mbali na kufanya vyema katika michuano hiyo yapili kwa ukubwa katika ngazi ya klabu msimu huu.
Kocha huyo alibainisha zaidi kuwa walikuwa na wachezaji wachache muhimu ambao walikosa mchezo wa mkondo wa kwanza. Hii ilitokana na majeraha na anaamini kikosi chake kitaongezewa nguvu na wachezaji hao
Tulikuwa na mfadhili miaka michache iliyopita ambaye alihama na kuondoka nchini na klabu iliyumba kutokea hapo. Hatukuweza kulipa mishahara na tuliporomoka katika suala la mafanikio na kupataka matokeo mabaya
Wananchi Yanga wanatafuta nafasi adhimu yakucheza fainali ya michuano ya Afrika hivyo ni Marumo Gallants pekee wamebaki kama kikwazo kwa Yanga kufikia ndoto yao.