Simba itampasa kuchanga vyema karata zake katika mchezo wa kwanza kama kweli wanataka kwenda nusu fainali kwani wataanzia nyumbani mchezo wa kwanza na kumalizia ugenini mchezo wa mwisho.
Kufuatia kipigo hicho kutoka kwa Raja klabu ya Simba sasa imepata ushindi katika michezo mitatu pekee kwenye kundi lao huku ikifunga mabao kumi na kuruhusu mabao saba.
Mchezo wa kwanza uliopigwa Jijini Dar es salaam Simba walikubali kipigo cha mabao matatu kwa bila mbele ya mashabiki wake na katika mchezo wa leo pia wamekubali kipigo cha mabao matatu kwa moja ugenini katika Jiji la Casablanca.