Mara nyingi Simba huwa wanamiliki mpira, huwezi kushindana nao kwenye hili. Kwa hiyo Yanga wanatakiwa kukaa nyuma na kuhakikisha wanafanya mashambulizi ya kushtukiza.
Hii ndiyo sherehe rasmi ya mpira wa miguu. Sherehe ambayo kila mtu hutamani kuishuhudia kwa jicho lake na kuisikia kwa masikio yake. Nchi nzima huwa inasimama kwa dakika 90 , presha hupanda kwa mashabiki wengi wa mpira wa miguu na hii ni kwa sababu moja tu. Timu hizi zimebeba mapenzi...
Kukubali kusikilizwa kwa Abdalah Shaibu "Ninja" kutakuwa na maana ya kwamba adhabu yake imeondolewa mpaka pale kamati ya nidhamu ya TFF itakapomsikiliza.
Kuwepo kwa Andrew Vincent "Dante" kwenye mechi kama hii dhidi ya timu yenye safu imara ya ushambuliaji kama Simba ni hatari kubwa sana kwa Yanga, hivo wanatakiwa kabisa kutoruhusu uwazi kutengenezeka katika eneo lao.
John Bocco yeye husimama katikati ya mabeki wawili muda mwingi. Unaposimama katikati ya mabeki wawili, mabeki huwekeza muda mwingi kwako, hivo kuacha uwazi eneo jingine la nyuma.
Tangu mwaka 1965, Simba na Yanga wamecheza mechi 101, Yanga akishinda michezo 36, sare 35 na kufungwa mechi 30. Simba akishinda michezo 30, akitoa sare mara 36 na kupoteza michezo 36. Yanga imejikusanyia alama 143 huku Simba ikijikusanyia pointi 125 katika michezo yote 101 waliyokutana, je Simba kupunguza “gap” la alama au Yanga kupanua gap hilo? tukutane taifa.
Chama cha soka mkoa wa Mwanza (MZFA) kimetolea ufafanuzi kuhusiana na kutokuwapo kwa gari la wagonjwa (Ambulance) kwenye uwanja wa CCM Kirumba wakati Mbao FC wakicheza na Coastal Union ya Tanga kwenye michuano ya Ligi Kuu soka Tanzania Bara. Katibu Msaidizi wa MZFA Khalid Bitebo amesema ni kweli gari la...