Wapo wale manguli ambao hawana hofu na lolote ana namba ya kudumu ndani ya timu amejiamini na kuaminika ana uhakika wa kuwepo yeye anachowaza ni dau kuongezeka tu kila msimu.
Walinzi wengine wa pembeni walioitwa katika kikosi cha Stars Kibwana Shomary [Yanga], Datius Peter [Kagera Sugar] na Yahya Mbegu wa Ihefu wote hawapo katika orodha hiyo.
Adel Amrouche aliyetangazwa hivi karibuni kupewa mikoba ya Stars amewajumuisha wachezaji wengi wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi akichanganya na baadhi wanaocheza Ligi ya ndani.