Ligi Kuu

Saba wa Yanga kuikosa Azam fc kesho

Sambaza....

Mabingwa wa soka Tanzania bara Yanga sc, kesho Jumamosi watakua ugenini kwenye uwanja wa Azam complex kuwakabili wenyeji wao Azam FC

Katika mchezo huo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, Yanga itawakosa nyota wake saba waliomajeruhi na mmoja akitumikia adhabu ya kuwa na kadi tatu za njano

Wachezaji hao ni Amis Tambwe, Yohana Oscar Nkomola, Abdallah Shaibu, Pato Ngonyani, Pius Buswita Donald Ngoma na Thabani Scara Kamusoko

Taarifa

Tarehe Muda Mwisho
90'

Hafsa habari wa klabu hiyo Dismas Ten, tayari ameweka wazi kuwa watawakosa nyota hao saba katika mchezo huo wa kesho

“Tutawakisa wachezaji wetu saba katika mchezo wetu wa kesho dhidi ya Azam FC, lakini wengine wapo tayari na mchezo huo ambao tutalazimika kushinda ili kujiweka vizuri kwenye msimamo wa ligi

Aidha pia klabu hiyo itamkosa kocha wake msaidizi Shadrack Nsajigwa, anayesafiri kwenda kwenye msiba wa shemeji yake, huku kibali cha kufanyia kazi cha kocha mkuu George Lwandamini ikiwa ni kitendawili

Endapo kitakosekana kibali hicho, ina maana Yanga kesho itaongozwa na mwalim wake wa viungo Noel Mwandila raia wa Zambia

PosTimuPWDLFAGDPts
1Simba SC173118401533996243394
2Yanga SC1651064118253104149359
3Azam FC167894434232125107311
4Kagera Sugar FC167525560145170-25211
5Tanzania Prisons164495956141153-12206
6Mtibwa Sugar FC165504966145167-22199
7Mbeya City FC165455763153184-31192
8Ruvu Shooting165455070146199-53185
9Coastal Union FC135434349112136-24172
10KMC FC134414251133137-4165
11Namungo FC9939312911910415148
12Mwadui FC108333243119134-15131
13Lipuli FC10733324298116-18131
14Biashara FC1062839398297-15123
15Mbao FC10730324586120-34122
16Polisi Tanzania9830303884104-20120

Sambaza....
Tafadhali tumia viungo vya mitandao ya jamii kusambaza.