Mashabiki wa Timu ya soka ya Yanga kutoka Tawi la Meatu lililopo wilayani Meatu Mkoani Simiyu wamesema licha ya baadhi ya Mashabiki kutoka timu pinzani kuwabeza kuwa ni ombaomba wanaamini kikosi hicho kilichopo chini ya kocha raia wa kongo Mwinyi Zahera kitachukua ubingwa wa ligi kuu bara msimu wa Mwaka 2018/19.
BAADA ya ushindi wa 16 katika michezo 18 ya mzunguko wa kwanza, pointi 50 mabingwa wa kihistoria wa ligi kuu Tanzania bara, Yanga SC wamesema wataifunga pia Azam FC katika mchezo wao wa mwisho wa mzunguko wa kwanza ili kutanua pengo lao la pointi.