Ni @heritier_makambo11 au @ambokile_10 kufunga kesho ili kumpita mwenzie katika jedwali la wafungaji bora tukielekekea nusu ya msimu pia? Fuatili tovuti yetu ambayo pia unaweza kuipata kwa app ya Android pekee.
Kocha wa timu ya soka ya Mbeya City 'Wanakomakumwanya' Ramadhan Nswanzurimo amesema hatoangalia rekodi ama michezo iliyopita watakapokwenda kucheza na Yanga siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.
Afisa Habari wa klabu ya soka ya Yanga Dismas Ten amesema maandalizi kuelekea katika mchezo wao wa Ligi dhidi ya Mbeya City yanaendelea vizuri na kwamba Kati ya wachezaji 20 ambao wamesafiri na timu hakuna ambaye anamajeraha yatakayomuweka nje ya mchezo huo.
KUELEKEA mchezo wao wa 18 msimu huu katika ligi kuu Tanzania bara msimu huu nahodha wa Yanga SC, Kelvin Yondan 'Vidic' amesema watapambana kama timu katika game yao vs Mbeya City FC wiki hii.
Katika ulimwengu wa Soka, ukisikia jina la “Jose Mourinho” kuna picha nyingi zinakujia kichwani, napicha hizo zinategemeana na jinsi unavyomkumbuka mreno huyo kwa kile alichoifanyia timu yako au kwa jinsi unavyolijua soka la dunia tangu akiwa Fc Porto na vilabu vingine.