Klabu ya soka ya Yanga baada yakupata ushindi wa mabao mawili kwa sifuri dhidi ya Namungo katika Dimba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es salaam wamefanikiwa kuandika rekodi nyingine mpya.
Baada ya ushindi huo sasa Yanga wamecheza michezo tisa na kufanikiwa kushinda yote mfululizo katika Ligi Kuu ya NBC na kuwa timu pekee kufanya hivyo katika Ligi Kuu Bara kwa msimu huu.
Yanga ilianza kupata ushindi Disemba nne mwaka jana dhidi ya Tanzania Prisons kwa bao moja bila wakiwa nyumbani na mpaka jana February nne dhidi ya Namungo wameendeleza wimbi la ushindi.
Katika michezo hiyo tisa Yanga wamefunga mabao kumi na saba na kuruhusu mabao mawili pekee katika mchezo dhidi ya Azam Fc uliomalizika kwa ushindi wa mabao matatu kwa mawili kwao. Yanga walipata matokeo katika michezo ifuatayo;
Yanga 1-0 TZ Prisons
Namungo 0-2 Yanga
Yanga 3-0 Polisi TZ
Yanga 3-0 Coastal Union
Azam Fc 2-3 Yanga
Mtibwa 0-1 Yanga
Yanga 1-0 Ihefu
Yanga 1-0 Ruvu Shooting
Yanga 2-0 Namungo fc
Baada ya mchezo wa Namungo sasa Yanga inaelekea katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika watakaocheza ugenini nchini Tunisia dhidi ya US Monastir.
Unaweza soma hizi pia..
AZIZ KI vs KIBU DENIS
Yanga na Simba zinakutana katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara ya NBC. Ikumbukwe katika mchezo uliopita klabu...
10/10 Wachezaji wa Yanga vs Mamelod
Mechi ya pili ya Robo Fainali Klabu Bingwa Afrika kati ya Mamelod Sundowns na Yanga ilisha kwa Mikwaju ya Penati,...
Yanga Baba Lao Afrika, Simba Mmmh!
vilabu vya Kaskazini vikiojekana kutawala katika nafasi za juu kwenye takwimu hizo zilizotoka
Yanga Ilivyosepa na Kijiji Msimbazi.
hakuwahi kupoteza mchezo hata mmoja wa Ligi lakini kipigo cha mabao matano kutoka kwa Mtani kimemfanya kupoteza kibarua chake