Ligi Kuu

Azam fc yaitandika Prisons 2-0

Sambaza....

Mabingwa wa kombe la mapinduzj klabu ya soka ya Azam FC, leo hii imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Prisons ya Mbeya, katika mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara

Katika mchezo huo ambao Azam FC, walikuwa ugenini kunako uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya

Haikuwa kazi nyepesi kwa Azam FC kuweza kuibuka na ushindi huo, kwani ilibidi wasubiri mpaka kunako dakika ya 70, ndipo mlinzi wake Yakub Mohammed alipoifungia bao la kwanza

Tano Bora ya Ligi Kuu Bara

PosTimuPWDLFAGDPts
1Simba SC1941334417382116266443
2Yanga SC1871254220307114193417
3Azam FC1911055036289141148365
4Tanzania Prisons183556563159175-16230
5Kagera Sugar FC182556067153188-35225

Wakati Prisons wakiendelea kutafakari namna ya kupata bao la kusawazisha, walijikuta wakifungwa bao la pili likiwekwa kimiani na mshambuliaji Paul Peter kunako dakika ya 83

Kwa ushindi huo waliopata Azam FC, unawafanya kufikisha alama 30, na kuwasogeza mpaka nafasi kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, wakiishusha Simba SC yanye alama 29, lakini wakiwa na mchezo mmoja mkononi ambapo kesho watakuwa ugenini kuikabili Kagera Sugar

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x