
Aliyewahi kuwa kocha mkuu wa klabu ya Yanga , Mwinyi Zahera amedai kuwa asilimia kubwa ya mashabiki wa Yanga wanampenda kwa kiasi kikubwa.
Akizungumza na kipindi cha mshikemshike cha Azam TV , Mwinyi Zahera amedai kuwa ukiwauliza mashabiki 100 wa Yanga basi mashabiki 98 wanampenda Mwinyi Zahera.
“Mashabiki wa Yanga wananipenda mpaka kufa. Ukizungumza na mashabiki 100 wa Yanga basi mashabiki 97 au 98 basi wananipenda sana” – alisema Mwinyi Zahera.

Mwinyi Zahera amedai kuwa kuna baadhi ya mashabiki wa Yanga wachache ambao walitumwa ili waje kumtukana yeye.
“Ni mashabiki wachache tu ambao hawanipenda. Ukiangalia kuna mashabiki walitumwa kuja kunitukana lakini baadaye walikuja kuniomba msamaha”-alimalizia Mwinyi Zahera.
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
Mbinu mpya za Yanga zilizoacha lawama kwa kipa wa Dodoma Jiji
Nasredeen Nabi ilimlazimu kutoka katika mfumo wake wa siku zote wa kumtegemea Fiston Mayele na kubadili mbinu ili kupata ushindi.