Kuifunga Simba , Yanga wanatakiwa kuwa na Manji, Zahera na Aussems kwa pamoja
Tarehe 4/1/2020 inakaribia sana. Siku ambayo nchi nzima itasimama kushuhudia pambano moja ambalo hugawa nchi pande mbili. Upande wa kwanza ni Yanga upande wa pili ni Simba. Hawa ndiyo wakubwa wa mpira hapa nchini na mechi yao hugusa hisia za watu wengi sana. Mechi hii inaonesha ni ya upande mmoja...