Hizi ni mechi za leo na kesho za mzunguko wa pili mzunguko wa 21. Kandanda tumekuwekea utabiri wetu wa kila mechi hapo chini. Unaweza kutupa na wewe pia
Mara ya mwisho kucheza na Mtibwa Sugar ilikuwa siku ambayo kulitokea sintofahamu kwenye klabu ya Simba baada ya kufungwa na Mtibwa Sugar kwenye michuano na Mapinduzi na Mohammed Dewji kutaka kujivua nafasi ya uenyekiti wa bodi ya Simba.
Kelele za mashabiki wa Simba kumtaka Patrick Aussems hazikuishia kwenye uwanja wa uhuru tu pale jana , inavyoonekana zimeenda mbali zaidi mpaka kwenye mitandao ya kijamii.
Dakika 45 za kipindi cha kwanza zilikuwa dakika nzuri sana kwa Polisi Tanzania . Dakika ambazo ziliwapa nguvu ya kuongoza kwa goli moja kwa bila huku wakikosa nafasi nyingi za wazi.
Walianza wao kufunga goli kipindi cha kwanza , goli ambalo liliwapa nguvu kubwa sana ya kutawala mchezo wa jana kwa dakika nyingi , Lakini dakika 5 za mwishoni zilileta maumivu na machozi.
Jana kulichezwa mechi Kali Kati ya Simba na Namungo FC. Kabla ya mechi hiyo Namungo FC walikuwa hawajawahi kupoteza hata mechi moja kwenye mechi tatu za mwisho walizocheza ugenini.
Washambuliaji Reliants Lusajo na Blaise Bigirimana ndio tishio zaidi kwenye kikosi cha Namungo ambapo kwa pamoja msimu huu wamefunga zaidi ya magoli 10.