Ligi Kuu

Hakuna pointi tatu za mezani kwa Yanga! lakini Arusha FC imepata.

Sambaza....

Kamati imekataa malalamiko ya Yanga kutaka ipatiwe ushindi wa pointi tatu na mabao matatu dhidi ya Mbeya City kwa timu hiyo kuwa na mchezaji zaidi kwenye mechi, kwa vile hakuna Kanuni yoyote ya Ligi Kuu inayoweza kubadili matokeo ya uwanjani kwa mazingira hayo.

Hakuna namna yoyote ile mchezaji anayezidi (extra player) kubadili matokeo ya mchezo. Katika mazingira ya extra player likifungwa bao, Mwamuzi atalikataa bao hilo. Kutokana na kanuni za Ligi kutojitosheleza katika suala hilo la extra player, Kamati iliangalia Kanuni za FIFA na kufikia uamuzi huo.

Ramadhan Malima (Kushoto), MBEYA CITY

Mchezaji Ramadhan Malima wa Mbeya City ambaye alitolewa nje kwa kadi nyekundu, lakini akatoka kwenye chumba cha kuvalia (dressing room) kwenda kushangilia bao la kusawazisha la timu yake amesimamishwa hadi suala lake litakaposikilizwa na Kamati ya Nidhamu TFF. Uamuzi wa kumsimamisha umezingatia Kanuni ya 9(5) ya Ligi Kuu kuhusu Usimamizi wa Ligi.

Kwa upande wa waamuzi, kulikuwa na upungufu katika suala la kusimamia ubadilishaji wa wachezaji (substitution), hivyo Kamati ya Waamuzi ya TFF imeandikiwa barua ili ichukua hatua dhidi ya wahusika. 

 

 

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x