Unai (Kocha wa ARSENAL)
EPL

Unafuu wa Wenger ni zaidi ya udhaifu wa Emery!

Sambaza....

Inawezekana tukafungwa michezo 3 mfululizo baada ya miaka mingi kwenye EPL.
Next game ni Jumapili ugenini vs Leicester City.

Tunaweza hii kiu ya kucheza UCL kupitia EPL ndio tukawa tumeikosa rasmi.
Maana tumebakiza michezo 3 kati ya hiyo mmoja pekee ndio tunacheza na Brighton & Hove Albion
Hawa Brighton sio wakubeza kwasababu wapo nafasi moja toka mstari wa kushuka daraja na jana tumeona walivyowasumbua Tottenham pale Tottenham Hotspur Stadium.

Arsene Wenger Kocha wa zamani wa Arsenal

Njia pekee ya sisi ARSENAL kucheza UCL msimu ujao ni kuchukua kombe la EUROPA LEAGUE vinginevyo ni bodi ya wakurugenzi wa klabu wampe mzigo wa maana Unai Emery wa kusajili wachezaji timamu na kikosi kipana ili tutengeneze mazingira ya kufanya vizuri kwenye EPL ili tushiriki UCL ya 2021/2022 panapo majaaliwa.

Je huku EUROPA LEAGUE tutawatoa Valencia ambao jana walikuwa na kiwango kizuri vs Atletico Madrid licha ya kupoteza huko Laliga.

Unafuu wa Wenger ni zaidi ya udhaifu wa Emery!

Big Daddy

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x