
Wekundu wa Msimbazi leo wamekata tiketi ya kucheza nusu fainali ya Sportpesa Supercup baada ya kuifunga Afc Leopard ya Kenya kwa mabao mawili kwa moja.
Achana na kuanza kwa pamoja kwa mafundi Cleotus Chama na Haruna Niyonzima, leo alikua ni Zana Coulibaly alieishika Taifa kwa shughuli pevu aliyoionyesha.
Tazama hapa jinsi “move” ya bao la kwanza lilivyofungwa kutoka pasi ya kwanza kutoka kwa Haruna Niyonzima mpaka kwa Emmanuel Okwi alipofunga bao la kwanza la Simba leo.

Licha ya kutengeneza bao la kwanza la Emmanuel Okwi katika dakika za mwanzo leo Coulibaly alikua katika kiwango cha juu huku mara kwa mara mashabiki walikua wakimshangilia kutokana na kasi yake ya kupeleka mashambulizi.
Tazama jinsi goli lilivyofungwa kwa picha.







Unaweza soma hizi pia..
Sevilla ndani ya Bongo!
Sevilla walioletwa nchini ni Sportpesa wanakuja kucheza na mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara Simba Sports Club mchezo wa kirafiki wa kimataifa nchini.
Ndemla aandaliwa kumthibiti Ever Banega Taifa!
Ndemla amekua akitumika kama kiungo wa chini kwa sasa na mwalimu Patrick Aussems hivyo basi katika mchezo dhidi ya Sevilla huenda akawa katika kikosi cha kwanza na kukutana na nahodha wa Sevilla.
Wapinzani wa Simba wamaliza Ligi kibabe
wamemaliza ligi kwa ushindi wa mabao mawili kwa sifuri na hivyo kujihakikishia nafasi ya kucheza Europa League.
Nyota wa kimataifa wa Taifa Stars ajiunga na matajiri wa Botswana.
Kiungo wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania Abdalla Hamis amejiunga na timu ya Orapa United FC ya nchini...