Martin Kiyumbi

Mchambuzi
Mchambuzi wa mpira wa miguu, mwenye Shahada ya Ualimu. Martin amejiunga na timu ya kandanda toka mwaka 2017, moja kati ya wachambuzi wakongwe katika familia yetu.
Ligi Kuu

Hivi Messi alikuwa mzito kwenye miguu ya Singano?

Ramadhani Singano "Messi", ndivyo tulivyoamua kumbatiza hilo jina baada ya kuhadaika na mguu wake wa kushoto. Mguu ambao alikuwa akiutumia vizuri kukokota mipira na kupiga vyenga ambavyo viliwafanya mashabiki kutoa tabasamu. Tabasamu ambalo lilikuja na ubatizo mkubwa kwa Ramadhani Singano, jina lake lilionekana halifai tena kutumika, Messi akawa mtu sahihi...
Blog

Zanzibar bado mnaikumbuka CECAFA?

Tulishuhudia CECAFA, macho yetu yalipendezwa na vingi vilivyotokea Kenya kwenye michuano ya CECAFA. Furaha ambayo ilipitiliza kiasi kwamba tulitumia kubeza sehemu moja na kusifia sehemu nyingine bila kutuliza akili zetu kwa umakini. Zanzibar ilisifiwa sana, Tanzania bara ilizodolewa sana, cha ajabu tulifika sehemu ambayo ilitulazimu kusema Zanzibar wana misingi imara...
Mabingwa Ulaya

Akili ya Kiitaliano iliamini kwenye miguu yenye Samba

Kwenye mechi kumi (10) kabla ya jana alikuwa amefanikiwa kufunga magoli mawili (2)pekee, hapana shaka tangu kifo cha mama yake kiwango chake kilikuwa cha kupanda na kushuka. Hakuwahi kusimama kwenye kiwango bora kwa muda mrefu mara baada ya mama yake kuachana naye na kwenda kwenye makazi yake ya milele. Alikaa...
Ligi Kuu

Singida United, anzeni walipokosea Mbeya City

Mapinduzi ya kizazi kipya cha watu kujivunia na kuzipenda timu zao za mikoani yalianzia kwa Mbeya City. Timu ambayo wana Mbeya walijivunia kuishabikia, kuipenda na kuisaidia kwa hali yoyote kadri ambavyo uwezo wao ulivyo waruhusu. Mbeya City hawakuwaangusha mashabiki wao mwanzoni, waliwapa furaha ambayo walitazamia kuipata kipindi ambacho wanaishabikia timu....
Ligi Kuu

Mahadhi wakumbuke Mazembe ujifunge masombo

Najua ushapitia nyakati tofauti zenye majira tofauti sana katika maisha yako, na kuna wakati mambo yako yalienda shoto na yakarudi upogo kwa sababu mbalimbali na kuna nyakati mambo yako yalitembea kwenye mstaari mnyoofu. Nyakati hizi zilikuwa na maana kubwa sana kwenye maisha yako kwa sababu maisha ya mwanadamu hukamilika kipindi...
Ligi Kuu

Zimbwe angusha uso kabla hujaenda Mvange

Inawezekana ndiye alikuwa mchezaji bora na muhimu katika kikosi cha Simba msimu uliopita. Aliifanya kazi yake bila kupumzika, kila mechi mguu wake ulikanyaga kila nyasi ya viwanja vyote vilivyoruhusiwa kwa ajili ya ligi kuu Tanzania bara. Lakini kwa sasa muda umechukua nafasi ya kufanya mabadiliko muda ni nafasi ya mabadiliko....
EPL

Hiki ndicho kilichosababisha Arsenal kuzidiwa na Spurs.

Tottenham Hotspurs katika mchezo huu walicheza mfumo wa 4-2-3-1 wakati Arsenal walicheza mifumo miwili ndani ya mchezo huu, mfumo wa kwanza ulikuwa 4-3-3 na mfumo wa 4-5-1 kwa nyakati tofauti. Wakati walipokuwa wanashambulia Arsenal walikuwa wanacheza mfumo wa 4-3-3 na walipokuwa wanajilinda walikuwa wanatumia wa 4-5-1 ambapo Ozil na Mkhtaryian...
EPL

Kwa leo Wembley utakuwa uwanja mgumu kwa Arsenal

Kwa miaka ya hivi karibuni North London Derby imekuwa na mvuto kutokana na Tottenham Hotspurs kuwa timu ya ushindani tofauti na miaka mingi ya nyuma. North London Derby ya 195 itakayopigwa katika uwanja wa Wembley, wanakutana kwa mara ya kwanza baada ya miaka 23. Mara ya mwisho timu hizi kukutana...
EPL

Upi ni udhaifu wa Bakayoko ?

Msimu jana Antonio Conte alikuwa anatumia mfumo wa 3-4-3, mfumo ambao ulimpa uhuru wa kuwatumia Kante na Matic kama viungo wa kati. Matic alicheza kama box to box midfielder na alifanikiwa kupiga pasi za mwisho za magoli zaidi ya saba katika ligi kuu ya England peke yake. Baada ya msimu...
1 73 74 75 76 77 79
Page 75 of 79