Ligi

Habari za Ligi Kuu maarufu Duniani Ligi Kuu (Premier League) hivyo hapa tunakuletea mkusanyiko wa uchambuzi na matukio yanayohusu Ligi Kuu pekee pamoja na Ligi Kuu Tanzania Bara (Ligi Kuu)

Ligi Kuu

Mikono Ya Kabwili Inapingana Na Hukumu Yetu Kwake

Nilikuwa naangalia marudio ya mechi ya Saint Louis na Yanga iliyochezwa Usherisheri. Katikati ya mechi nilibaki naangalia umbo la golikipa wa Yanga, Youthe Rostand. Umbo ambalo linamfaa golikipa yoyote kuwa nalo. Kimo chake kizuri , kimo kinachompa sifa ya ziada kama golikipa. Kuwa na umbo zuri hakutoshi kukufanya kuwa golikipa...
Ligi Kuu

Simbasc Yatakata, Yaendela Kujichimbia Kileleni

Simba sc, imeisambaratisha Mbao FC kwa mabao 5-0 na kuendelea kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya soka Tanzania bara, maarufu kama Vodacom Premier League Mchezo huo uliofanyika kunako uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Simba walijipatia bao la kwanza kunako dakika ya 37, kupitia kwa Shiza Kichuya...
Ligi Kuu

Hivi Messi alikuwa mzito kwenye miguu ya Singano?

Ramadhani Singano "Messi", ndivyo tulivyoamua kumbatiza hilo jina baada ya kuhadaika na mguu wake wa kushoto. Mguu ambao alikuwa akiutumia vizuri kukokota mipira na kupiga vyenga ambavyo viliwafanya mashabiki kutoa tabasamu. Tabasamu ambalo lilikuja na ubatizo mkubwa kwa Ramadhani Singano, jina lake lilionekana halifai tena kutumika, Messi akawa mtu sahihi...
EPL

Pep Guardiola ashitakiwa Uingereza

Meneja wa klabu wa klabu ya Manchester City, Pep Guardiola, ameshatakiwa na chama cha soka cha Uingereza (FA) kwa kosa la kuvaa riboni yenye ujumbe wa kisiasa Meneja huyo alivaa riboni hiyo, kwenye mchezo wa kombe la FA dhidi ya Wigan Athletic ambapo alipoteza kwa kufungwa bao 1-0 na kuondolewa...
Ligi

Infantino afurahia mabadiliko TFF

Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF, ndugu Wallace Karia, amemkabidhi kinyago kilichochongwa Tanzania rais wa Shirikisho la soka Duniani FIFA Giann Infantino aliyekuwa nchini kuendesha mkutano wa FIFA wa maendeleo ya mpira ujulikanao (Fifa football executive summit) Mkutano huo uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Julius Nyerere international convention...
Ligi Kuu

Singida United, anzeni walipokosea Mbeya City

Mapinduzi ya kizazi kipya cha watu kujivunia na kuzipenda timu zao za mikoani yalianzia kwa Mbeya City. Timu ambayo wana Mbeya walijivunia kuishabikia, kuipenda na kuisaidia kwa hali yoyote kadri ambavyo uwezo wao ulivyo waruhusu. Mbeya City hawakuwaangusha mashabiki wao mwanzoni, waliwapa furaha ambayo walitazamia kuipata kipindi ambacho wanaishabikia timu....
Ligi Kuu

Mahadhi wakumbuke Mazembe ujifunge masombo

Najua ushapitia nyakati tofauti zenye majira tofauti sana katika maisha yako, na kuna wakati mambo yako yalienda shoto na yakarudi upogo kwa sababu mbalimbali na kuna nyakati mambo yako yalitembea kwenye mstaari mnyoofu. Nyakati hizi zilikuwa na maana kubwa sana kwenye maisha yako kwa sababu maisha ya mwanadamu hukamilika kipindi...
Ligi Kuu

Lipuli FC yaigomea Azam FC

Mabingwa wa kombe la mapinduzi Azam FC, imeshindwa kuonesha cheche zake baada ya kutoka sare ya bila kufungana na Lipuli FC katika mchezo wa ligi kuu bara Mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la Samora mjini Iringa, ulikuwa na ushindani mkubwa kwa dakika zote tisini Kwa matokeao hayo yanaifanya Azam kujikusanyia...
Ligi Kuu

Azam fc kuendeleza ubabe kwa Lipuli fc hii leo?

Ligi kuu ya soka Tanzania bara kuendelea tena hii leo kwa mchezo mmoja kupigwa kunako dimba la Samora mjini Iringa, amabo mabingwa wa kombe la Mapinduzi Azam FC watakuwa wageni wa Lipuli FC Mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkali kutokana na rekodi za timu zote katika michezo ya hivi...
Ligi Kuu

Zimbwe angusha uso kabla hujaenda Mvange

Inawezekana ndiye alikuwa mchezaji bora na muhimu katika kikosi cha Simba msimu uliopita. Aliifanya kazi yake bila kupumzika, kila mechi mguu wake ulikanyaga kila nyasi ya viwanja vyote vilivyoruhusiwa kwa ajili ya ligi kuu Tanzania bara. Lakini kwa sasa muda umechukua nafasi ya kufanya mabadiliko muda ni nafasi ya mabadiliko....
1 107 108 109 110 111 118
Page 109 of 118