EPL

Nini tatizo la Chelsea Msimu huu?

Sambaza....

Msimu jana ulikuwa msimu wa kwanza kwa kocha Antonio Conte akiwa Chelsea. Pamoja na kwamba ulikuwa msimu wake wa kwanza akiwa kama kocha wa Chelsea, na msimu wa kwanza kwake akiwa kwenye nchi ya England lakini alifanikiwa kuchukua ubingwa wa ligi kuu ya England.

Antonio Conte aliikuta Chelsea ikiwa imefanya vibaya msimu mmoja kabla ya kuja yeye.

Lakini alifanikiwa kufanya vizuri, na timu yake kuchukua ubingwa wa ligi kuu.

Lakini msimu huu imekuwa tofauti na msimu jana, mpaka sasa iko nafasi ya tatu kwenye msimu wa ligi kuu ya England.

Na jana tumeshuhudia ikitolewa katika michuano ya kombe la ligi ( EFL) Katika hatua ya nusu fainali na Arsenal.

Kipi kinafanya Chelsea iwe na mwenendo wa kusuasua msimu huu tofauti na msimu jana ??

Chelsea ni timu ya mtu mmoja, mtu huyu akiwa hayupo Chelsea huyumba na wakati mwingine hata akiwepo na asipocheza vizuri timu nayo hucheza vibaya na kuhangaika kupata matokeo.

Image result for Sad conte

Pamoja na kwamba Hazard amekuwa tegemeo kubwa kwa misimu mingi pale Chelsea ila msimu huu amekuwa tegemeo kubwa sana kutokana na wenzake wanaomzunguka kuwa katika viwango visivyo bora.

Willian na Pedro wamekuwa wakitumika kama suluhisho kipindi ambacho Hazard akiwa hayuko katika kiwango kizuri.

Matokeo ya Ligi Kuu

Msimu huu imekuwa tofauti, Willian na Pedro wameshuka kiwango na hii inakuwa inaipa shida Chelsea inapokuwa haina Hazard au Hazard akiwa hayuko vizuri anakosekana mtu wa kuyaziba madhaifu yake.

Vipi usajili wa Antonio Conte katika dirisha la majira ya joto lililopita ulikuwa na faida kwenye timu ?

Mpaka sasa hakuna kitu kikubwa alichonufaika nacho kutoka kwa wachezaji aliowaleta msimu huu.

Wachezaji wote waliokuja msimu huu katika timu ya Chelsea hawajazoea ligi hali ambayo inawafanya wasitoe mchango mkubwa wa moja kwa moja kwenye timu.

Pamoja na kwamba Morata mpaka sasa ameshafanikiwa kufikisha magoli 12 lakini anakosa hali ya kuibeba timu wakati mgumu.

Image result for morata

Na hii inachangia kwa kiasi kikubwa na ugeni wa ligi, kama ilivyo kwa wenzake kina Zappacosta na Rudiger.

Kama Alvaro Morata anakosa uwezo mkubwa wa kuibeba timu nyakati ngumu na alisajiliwa kwa ajili ya kuziba pengo la Diego Costa , ndiyo ina maanisha hakuwa mtu sahihi wa kuziba pengo la Diego Costa?

Kuna ukweli kwenye hili swali, kwa sababu Diego Costa ni mpambanaji zaidi ya Alvaro Morata, alikuwa anapambana hata wakati ambao Chelsea ilikuwa inaonekana imeshikwa lakini alikuwa na uwezo wa kuiokoa Chelsea katika nyakati ngumu hii ni tofauti na kwa Alvaro Morata.

Msimu jana tulimuona Antonio Conte akija na mfumo wa 3-4-3 na kufanikiwa kuchukua ubingwa , vipi msimu huu kwanini imekuwa ngumu kwake kutumia mfumo huu na kuendelea kuwa tishio kwa wapinzani wake?

Baada ya kufungwa goli 3-0 na Arsenal msimu jana Antonio Conte aliamua kubadili mfumo kutoka mfumo wa kutumia mabeki wanne mpaka mfumo wa kutumia mabeki watatu

Timu iliimarika mpaka timu ikashinda michezo 12 mfululizo ikawa rekodi ya klabu.

Msimu huu imekuwa tofauti na msimu jana, msimu huu amebadilika kutoka katika mfumo wa 3-4-3 mpaka katika mfumo wa 3-5-2 ili aweze kuwachezesha kwa pamoja Kante, Bakayoko na Fabregas katika eneo la katikati mwa uwanja.

Mfumo wake huu umekuwa na changamoto tatu.

Changamoto ya kwanza , ni aina ya wachezaji ambao alikuwa nao msimu jana na msimu huu ni tofauti.

Kwa sababu msimu jana eneo la katikati walikuwa na Kante pamoja na Matic.

Matic alicheza kama box to box middfielder, ambapo alijitahidi kuleta uwiano mzuri wa kushambulia na kuzuia , alimaliza msimu akiwa na pasi saba (7) za mwisho za magoli.

Msimu huu imekuwa tofauti Bakayoko pamoja na kwamba amekuwa akifanya vizuri timu inapokuwa inazuia lakini timu ikiwa inashambulia amekuwa akifanya vibaya kwa kukosa nafasi nyingi za wazi pia siyo mbunifu wa kutoa pasi za mwisho za magoli.

Bakayoko (Kulia)

Tatizo la pili ni wachezaji wa mbele kushuka viwango tofauti na msimu jana. Pedro na Willian msimu jana walikuwa msaada mkubwa sana katika mfumo huu lakini msimu huu imekuwa tofauti.

Tatizo la tatu, makocha wengi wameshajua mbinu za kupambana na mfumo wa kutumia mabeki watatu, ndiyo maana hata wenyewe wameanza kuutumia mfumo huu.

Antonio Conte amekuwa akilalamika kuwa kikosi chake kinakumbwa na uchovu , hii inaweza ikawa na ukweli ndani yake ?

Ndiyo, msimu jana Chelsea alikuwa na michuano michache, alitoka mapema EFL, akabaki na FA Cup pamoja na Ligi kuu ambapo FA Cup nayo hakufika mbali.

Hivo EPL lilikuwa kombe pekee alilowekeza nguvu kubwa.

Msimu huu ana michuano mingi ambayo amewekeza nguvu kubwa kwa kikosi hicho hicho, kikosi anachokitumia ligi kuu ya England ndicho hicho hicho anachokitumia EFL, FA Cups na ligi ya mabingwa barani ulaya.

Hivo kwa ufinyu huu wa kikosi unawafanya wachezaji wapate uchovu, mchezaji akipata uchovu kasi yake ya kupigana hupungua kwa kiasi kikubwa

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x