Blog

Saido Mane apagawa na Diamond Platnumz !

Sambaza....

Jana kulikuwa na halfa ya utoaji tunzo za soka barani Afrika zinazoandaliwa na shirikisho la soka barani Afrika (CAF) ambapo tulishuhudia mchezaji wa Senegal na Liverpool ya England akiibuka kuwa mchezaji bora wa Afrika kwa mara ya tatu mfululizo.

Katika halfa hiyo , mwanamuziki wa Tanzania,  Diamond Platnumz aliarikwa kwenda kutumbuiza kwenye hafla hiyo ya utoaji tunzo. Mwanamziki huyo alikonga nyoyo za watu mbalimbali.

Wakati anatumbuiza watu mbalimbali walipanda jukwaani kucheza na kwa pamoja na Diamond Platinumz aliyekuwa anatumbuiza wimbo wa Yope Remix.

Saido Mane alishindwa kujizuia na kupanda jukwaani wakati Diamond anatumbuiza , pamoja na Saido Mane , watu wengine waliopanda walikuwa ni pamoja na raisi wa FIFA , Gianni Infantino , Samuel Etoo na wengine wengi.

Sambaza....