
Leo kutakuwepo na mchezo wa ligi kuu kati ya Simba na Alliance ya Mwanza katika uwanja wa CCM kirumba.
Akizungumza na mtandao huu msemaji wa Alliance Jackson Mwafulango amedai kuwa Simba kesho lazima auliwe kwa sababu amepotea njia.
Jackson Mwafulango amedai kuwa walienda kuweka kambi Kenya kwa ajili ya kuwaua Simba na Simba wanatakiwa kujiandaa kwenye hilo.
“Tumeenda Kenya kwa ajili ya kuweka kambi bora na nzuri kwa ajili ya kuwaua Simba hivo wanatakiwa wajiandae vizuri”.
Akizungumza kuhusu timu yake kufanya vibaya kwenye uwanja wa CCM kirumba ukilinganisha na uwanja wa Nyamagana amedai kuwa wamejifunza.
” Tumejifunza na tunataka kuwaonesha Simba kwa sasa uwanja huu na tutafanya vizuri kwenye mechi hii inabidi wajiandae”
Unaweza soma hizi pia..
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.
Alli Kamwe: Kumbe bila moto wanateseka!
: Asante Moalin. Asante Pablo Franco, Mechi ilichezwa sana kwenye mbinu kisha ikamalizikia kwenye Ufundi wa wachezaji.