Fabrice Ngoma (katikati)
Stori

Simba Yapewa Ratiba Mpya na CAF

Sambaza....

Shirikisho la Soka barani Afrika hatimaye limetangaza maelezo ya Super Ligi ya Afrika, ambayo sasa inaitwa Ligi ya Soka ya Afrika, ambayo itajumuisha wanachama wanane, ikiwa ni pamoja na Simba Sc ya nchini.

Ligi kuu ya CAF ilikuwa imepigiwa upatu kwa muda mrefu na CAF wamethibitisha kuwa mechi hizo zitafanyika kati ya Oktoba 20 na 11 Novemba 2023. Timu zitakazoshiriki ni Al Ahly Football Club, Espérance Sportive de Tunis ya Tunisia, Wydad Athletic Club, Enyimba Football Club, Tout Puissant Mazembe, Atlético Petróleos de Luanda na Mamelody Sundowns.

 

Michuano hiyo itaendeshwa kwa mfumo wa mtoano kutoka timu nane shiriki, robo fainali, nusu fainali mbili na fainali (zote zilichezwa kwa michezo miwili).

Taarifa ya CAF ilisema ” Droo ya michuano hii itafanyika September 2 Cairo, Misri saa moja usiku.”

“Michuano hii ya kihistoria itafanyika  kwa muda wa wiki nne, ikianza kwa sherehe za ufunguzi na mechi ya kwanza tarehe 20 Oktoba 2023 jijini Dar es Salam, Tanzania,” ilisema taarifa hiyo.

Kikosi cha Simba kilichoshiriki michuano ya Kimataifa msimu uliopita.

Michuano hiyo inachukua nafasi kati ya October 20 na November 11 mwaka huu na rasmi imethibitika mwakani michuano hiyo ya Super ligi itashirikisha timu 24 kutoka kanda zote za Afrika.

Mchezo wa fainali unatarajiwa kupigwa kati ya November 5 na 11 mwaka huu. Sasa ni wazi Wekundu wa Msimbazi wana kibarua kikubwa katika michuano hii mipya na kuweka historia mpya.

 

Sambaza....