
Baada ya habari nyingi za Yanga kutaka kumchukua Patrick Aussems kuwa kocha mkuu wa klabu ya Yanga, Leo hii Afisa Habari Wa Yanga Hassan Bumbuli ametoa siri ambayo wengi tulikuwa hatuijui.
Hassan Bumbuli amesema kuwa kocha mpya wa Simba Sven Van Den Broeck alianza kuitaka Yanga lakini Yanga walimkatalia na akaamua kutuma maombi kwenye klabu ya Simba.
“Sven Van Den Broeck alituma maombi ya kazi kwetu Baada ya Mwinyi Zahera kutimuliwa , sisi tulimkataa na tulimpomkataa aliamua kuomba kazi kwenye klabu ya Simba Baada ya sisi kumkataa”. Alisema Afisa Habari huyo wa Yanga. Yanga bado inatafuta kocha mpya ambaye ataziba pengo la Mwinyi Zahera
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.