
Zana
Mchezaji wa Zamani wa klabu ya Simba, Zana Oumary Coulibaly leo amejiunga rasmi na klabu ya AS Club Vita ya Kinshansa nchini Congo kwa mkataba ambao bado haujawekwa wazi.
Zana ambaye aliitumikia Simba kwa nusu Msimu amepata dili hilo baada ya kutemwa na wekundu hao wa Msimbazi kutokana na kushindwa kuvaa viatu vya Shomari Kapombe kisawasawa baada ya kupata majeraha kati kati ya msimu.
Zana atakumbukwa zaidi na jamii ya wana Simba kutokana na muonekano wake wa kipekee, ukaribu na mashabiki , vituko na aina ya uchezaji wake wa kupiga krosi yaani kumwaga maji na yakamwagika.
Kandanda inamtakia kila la heri, Zana Coulibaly katika changamoto yake mpya.
Unaweza soma hizi pia..
Simba na Yanga kukutana tena mwezi huu.
Ratiba ya kombe la Azamsports Federation Cup imetolewa leo na Shirikisho la Soka nchini TFF huku pia wakitaja na viwanja vitakavyotumika katika michezo hiyo ya nusu fainali.
Kombe la FA: Ni fainali ndani ya fainali.
Mchezo wa nusu fainali ni utakua na hadhi, ukubwa na umaarufu kuliko fainali yenyewe kutokana na aina ya wapinzani watakaokutana.
Vigogo wa Afrika wanalakujifunza kwa Simba hii!
Simba licha ya kutolewa katika robo fainali ya klabu bingwa Afrika mara mbili na Shirikisho mara moja lakini bado hakupoteza nyumbani
Yametimia wanakutana tena
Tangu kombe hili lirudi Simba amekua na historia nzuri mbele ya mwenzake, katika michezo mitatu yote Simba ameshinda