David Molinga "Falcao"
Tetesi

David Molinga kutemwa Yanga

Sambaza....

Baada ya Jana David Molinga kutoonekana hata kwenye orodha ya wachezaji wa akiba wa Yanga na kuacha maswali mengi kuhusiana na tukio hilo kuna Habari kuwa uongozi wa Yanga wanampango wa kuachana na mchezaji huyo.

Mchezaji huyo ambaye yuko kwa mkopo katika klabu hiyo ya Yanga ,inaelezewa kuwa viongozi mbalimbali wa Yanga wamechoka na tabia zake za utovu wa nidhamu na wanampango wa kuachana naye , David Molinga aliletwa na aliyewahi kuwa kocha wa Yanga , Mwinyi Zahera .

Sambaza....