Tetesi

Kichuya na Ajib kutemwa SIMBA

Sambaza....

Baada ya Yanga kuachana na wachezaji 14 mahasimu wao wakubwa Simba nao wanampango wa kuachana na baadhi ya wachezaji katika kikosi chao.

Taarifa za ndani zinaainisha kuwa wachezaji saba ndani ya kikosi cha Simba wataachwa kutokana na sababu mbalimbali.

Taarifa hii imeanisha wachezaji ambao wataachwa ni Ibrahim Ajib ambaye kabla ya kuja Simba aliwika akiwa katika klabu ya Yanga, wachezaji wengine ambao inasemekana wataachwa ni Haruna Shamte , Shiza Kichuya , Rashid Juma, Yusuph Mlipili, Sharaf Shiboub, Tairon Da Silva

Sambaza....