Ligi Kuu

Mnyama atakata Njombe, aikimbia Yanga!

Sambaza....

Klabu ya SimbaSc ya Dar es salaam imeendeleza wimbi la ushindi katika ligi kuu  (VPL) baada ya kuifunga Njombe Mji ya Njombe kwa mabao mawili kwa sifuri.

Mchezo huo uliokua mgumu kwa pande zote mbili, huku kila timu ikipambana kupata matokeo ili kujiweka nafasi nzuri katika ligi kuu Bara.

Simba vs Yanga Msimamo

#TimuPWDLFAGDPts
1168114391532693233381
2160103401723997142349
3163864433224121103302
4163515557144161-17208
5161466055134150-16198

Alikua ni John Raphael Bocco “Mr Captain” alieamua mchezo huo baada ya kufunga mabao yote mawili na kuipa ushindi muhimu timu yake ya SimbaSc katika harakati za kuusaka Ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu.

Bocco alifunga goli la kwanza katika dakika ya 17 baada ya kupokea mpira mrefu uliopigwa na Yusuph Mlipili kabla ya kuutuliza na kupiga shuti kali nje ya 18. Mnamo katika dakika ya 68 Bocco tena alipokea pasi safi kutoka kwa Shomari Kapombe na kuukwamisha mpira wavuni.

Mpaka dakika 90 zinamalizika Njombe Mji 0 SimbaSc 2. Kwa matokeo hayo yanaifanya Simba kufikisha pointi 49 na kuwaacha Yanga wakiwa na point 46 akifwatiwa na Azam mwenye point 42.


Sambaza....
Tafadhali tumia viungo vya mitandao ya jamii kusambaza.