
Kocha mkongwe Juma Mwambusi yuko njiani kuelekea kutambulishwa kama kocha msaidizi wa klabu ya Yanga ambapo atakwenda kufanya kazi na kocha mkuu raia wa Burundi.
Mwambusi msimu uliopita alikua akihudumu kama kocha mkuu wa Mbeya city kabla ya kutupiwa virago itakua si mara yake ya kwanza kufanya kazi na Wanajangwani hao. Ikumbukwe Mwambusi alihudumu Yanga kama kocha msaidizi chini ya Hans Plujim.
Benchi la ufundi la Yanga litakua chini ya Cedrik Kaze (Kocha Mkuu), Juma Mwambusi (Kocha Msaidizi), Vladmir Niyonkuru (Kocha wa makipa) na Hafidh Saleh (Meneja).
Utambulisho wa benchi jipya la ufundu unatarajiwa kufanyika hivi karibuni kabla ya kufikia lilele cha siku ya Mwananchi Jumapili August 30.
Unaweza soma hizi pia..
Mbinu mpya za Yanga zilizoacha lawama kwa kipa wa Dodoma Jiji
Nasredeen Nabi ilimlazimu kutoka katika mfumo wake wa siku zote wa kumtegemea Fiston Mayele na kubadili mbinu ili kupata ushindi.
Simba na Yanga kukutana tena mwezi huu.
Ratiba ya kombe la Azamsports Federation Cup imetolewa leo na Shirikisho la Soka nchini TFF huku pia wakitaja na viwanja vitakavyotumika katika michezo hiyo ya nusu fainali.
Kipa Dodoma katolewa tuu kafara!
Ndani ya miaka miwili unataka kuniambia ameisha kabisa? Je hatupaswi kumshukia kocha wake wa makipa?
Alli Kamwe: Yanga imeifunga Yanga B!
Bao la 2 la Yanga ni OFFSIDE. Kama Shuti la Mauya lingekwenda moja kwa moja, hakuna tatizo.