
Ngassa
Kiungo mshambuliaji wa Yanga Mrisho Ngassa maarufu kama “Uncle” ameamua kuwaaga mashabiki na klabu yake ya Yanga kwa ujumla kutokana na kuandika maneno katika ukurasa wake wa Instagram unaoashiria msimu ujao hatokua tena mchezaji wa Yanga.
Ngassa ama “Enjoy soccer” inaonekana ni miongoni mwa wachezaji 13 ambao Yanga inatarajiwa kuachana nao katika kipindi hiki baada ya Ligi kumalizika.

“Kwanza nitoe shukrani zangu kwa wote tuliokuwa pamoja katika kipindi chote, Yanga viongozi wangu mashabiki na wachezaji wenzangu kwa kikao kilichofanywa leo sitakuwa katika kikosi cha Yanga niwatakie mafanikio yalio mema. Enjoy soccer.” Ameandika Uncle Ngassa katika ukurasa wake wa Instagram.
Unaweza soma hizi pia..
Mbinu mpya za Yanga zilizoacha lawama kwa kipa wa Dodoma Jiji
Nasredeen Nabi ilimlazimu kutoka katika mfumo wake wa siku zote wa kumtegemea Fiston Mayele na kubadili mbinu ili kupata ushindi.
Simba na Yanga kukutana tena mwezi huu.
Ratiba ya kombe la Azamsports Federation Cup imetolewa leo na Shirikisho la Soka nchini TFF huku pia wakitaja na viwanja vitakavyotumika katika michezo hiyo ya nusu fainali.
Kipa Dodoma katolewa tuu kafara!
Ndani ya miaka miwili unataka kuniambia ameisha kabisa? Je hatupaswi kumshukia kocha wake wa makipa?
Alli Kamwe: Yanga imeifunga Yanga B!
Bao la 2 la Yanga ni OFFSIDE. Kama Shuti la Mauya lingekwenda moja kwa moja, hakuna tatizo.