
Harrison Mwakyembe waziri mwenye dhamana ya michezo!
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe amezungumaza na kituo cha redio cha Efm katika kipindi cha michezo na kuweka wazi jinsi alivyomuulizia nyota wa DR Congo David Molinga.
Katika mchezo uliowakutanisha JKT Tanzania dhidi ya Yanga katika dimba la Jamuhuri Dodoma Jumatano June 17 ambapo matokeo yalikua sare kwa bao moja kwa moja, Mh. Mwakyembe alikuepo uwanjani hapo kuushuhudia.

Mwakyembe amesema:”Unajua timu za jeshi hazina mapumziko, wao kipindi cha Corona hakuna Corona lazima wawe fiti kwa kufanya mazoezi sasa nilishangaa nilipoona kikosi cha Yanga hakina Molinga.
“Niliwauliza wale ambao nilikuwa nao, jamani mbona Molinga hapa simuoni akianza ila baadaye kidogo nilimuona akiingia, wale ni wanajeshi lazima kikosi kitakachopambana nao kiwe na nguvu muda wote.”

Katika mchezo huo JKT ndio waliokuwa wakwanza kupata bao kupitia kwa Michael Aidan kabla ya Patrick Sibomana kusawazisha kipindi cha pili. Pia ilishuhudiwa vurugu kubwa mchezo ulipokua unaelekea mwishoni na kupelekea Mwinyi Kazimoto na Lamine Moro kuonyeshwa kadi nyekundu.
Unaweza soma hizi pia..
Azam kujimaliza yenyewe mbele ya Simba!
Miongoni mwa maeneo yatakayopa ushindi Simba katika mchezo huo ni eneo la kiungo na eneo la mlinda mlango.
Kola tishio jipya kwa Onyango na Inonga
Hazikupita siku nyingi Mayele akakutana na Simba na kutiwa mfukoni na Mcongo mwenzake Inonga Baka na kupeleka kuzima mtetemo wake
Mbinu mpya za Yanga zilizoacha lawama kwa kipa wa Dodoma Jiji
Nasredeen Nabi ilimlazimu kutoka katika mfumo wake wa siku zote wa kumtegemea Fiston Mayele na kubadili mbinu ili kupata ushindi.
Simba na Yanga kukutana tena mwezi huu.
Ratiba ya kombe la Azamsports Federation Cup imetolewa leo na Shirikisho la Soka nchini TFF huku pia wakitaja na viwanja vitakavyotumika katika michezo hiyo ya nusu fainali.