Spocha

Saa02Asb: Alama Nyingi kwa Msimu Mmoja.

Sambaza....

Manchester City ndio timu pekee katika historia ya Ligi kuu Uingereza kuwahi kufikisha alama 100 kwa msimu, walifanya hivyo katika msimu wa 2017/2018.

Katika mwaka huo huo walichukua ubingwa kwa umbali wa alama 19 toka mshindi wa pili, alama nyingi zaidi katika historia ya Ligi kuu Uingereza,  walikusanya alama nyingi za ugenini (50), nyingi kuliko timu yoyote katika historia ya ligi hiyo. Lakini pia waliweka rekodi ya kushinda michezo mingi ya ligi (32) katika msimu hio wa 2017/18.


Sambaza....