
Imeripotiwa kwamba Mshambualiaji wa Zamani wa Barcelona na Inter Milan Samuel Eto’o amemuahidi kumnunulia Nyumba nahodha wa zamani wa Timu ya Taifa ya Cameroon Norbert Owona.
Eto’o amefikia maamuzi hayo baada ya Nyota huyo aliyewika na Cameroon katika miaka ya 1960 na 1970 kuripotiwa kwamba hana pa kuishi akiwa na umri wa miaka 67, anaishi kwenye mitaa ya mji wa Douala.
Hivi karibuni Owona alilazwa hospitalini kutokana na Kuugua ugonjwa wa hernia na Eto’o alipomtembelea ndipo akamuahidi kumnunulia nyumba nyote Huyo.
Mbali na hilo pia Eto’o amechanga zaidi ya shilingi Milioni 1.7 kwa ajili ya matibabu ya nahodha huyo katika Mchango maalumu unaoendeshwa na nyota mwingine wa Zamani wa Cameroon Joseph Kamga.
Unaweza soma hizi pia..
Waandishi wa habari za michezo waigalagaza Unitalent.
Unitalent hawakuishia tuu kufungwa mabao mawili lakini pia waliteseka uwanjani haswa katika eneo la kiungo
Kwanini Boban Hakuyapenda Maisha Ya Ulaya…?
Yumkini Haruna Moshi alishawishiwa kutokukipenda ambacho kingemsaidia maishani. Soma stori hii
Manara: Tunataka kuujaza uwanja Jumamosi!
Msemaji huyo pia ameonyesha ni kwa kiasi gani wamedhamiria kuujaza uwanja huku akitangaza neema kwa mashabiki wa Yanga wataokata tiketi kwenda uwanjani.
Hivi ndivyo tulivyomuua Samatta wetu.
Mimi siyo mpenzi wa mpira wa miguu ila nilisikia Rafiki zake wakimwiita Ronaldinho Gaucho,