Blog

HELL BIG NO!

Sambaza....

Mambo yanatokea kwa haraka sana! Kutoka HAWAAMINI MACHO YAOOOO Hadi hatumtaki Matola.

Hapana hii sio SAWA! Hili sio Simba lile Niliwahi kusema LINAPIGA PIRA BIRIANI na Nyote mkaitikia kila Mitaa kwa Kusema SPONGA PIRA BIRYANI!

Nawaambia hii Selemani Matola ni Muajiriwa wa Simba Sponga Waajiriwa Wote wana namna yao ya Kuingia na Kutoka katika Ajira zao!.

Hivi Hii Sumu ya Kukataa Watu wetu Imezalishwa na nani? HEBU TULIENI BASI WANANGU VITA AKILI!

Waswahili wanasema Kamba Hukatikia Pembamba kweli ila WASHABIKI wa Simba Sponga ninaowajua mimi ni Wakubwa kuliko huu Ujinga tulioufanya leo pale Lupaso!

Nyie washabiki wa Sponga Mbona Mnasahau Mapema sana? Sponga Lililokasirika, Sponga Lililotoa Meno, Sponga Lililotoa Makucha yake Nje!

Nyie Sponga linalopiga MIPASI HADI UKWENI leo hii Mashabiki mnakuja kuimba Nyimbo zisizo RASMI! Leo mnakuja Kuimba Nyimbo ambazo zitakuja Kutumika kutuumiza?

Kuna vitu haviwezi kuwa Sawa ndio lakini Mambo ya Familia huwa yanamalizwa ndani kwa Familia!

PosTimuPFAGDPts
13061184378
23074175773
33054292559
4303426853

Mechi ya Tatu, Pointi Saba, Hatujafungwa, Still ndio Timu iliyofunga Magoli mengi na kufungwa Machache sasa Je Tungekuwa kama Timu ya Mjomba wang Msolopa Timu Yake Imecheza Mechi 6, wana Pointi Moya na Shabiki ni Mmoya ambae ni yeye tu huyo Mjomba wangu na hajaanza Kutukana Bodi yao Imfukuze Kocha!

Jana jamaa zetu wamedroo Yes! “Wamedroo kwa kutumia Banda la Mpesa la Mjomba wangu MSOLOPA Hadi Kumbukumbu Namba ya Muamala ninayo!”

Hebu Tulieni wanangu Kama safari ndio kwanza tupo hatua ya TATU! tuna Mwendo Mrefu yapo yanayo rekebishika na yapo ya kusubiri Dirisha Dogo kurekebishika!

Hizi Nyimbo zenu zitunzeni Wanangu maana Kesho tunatoa Ngoma Mpya kama Sita chini ya King Faida hapa Lilongwe Malawi Tulieni Wanangu kwani hamjui hili Mtu aso Akili pekee ndio hujificha kwenye Shamba la Karanga!

Narudia tena SPONGA LILILO KASIRIKA LIMETOA MENO NA MAKUCHA YOTE YAKO NJE NI UNSTOPPABLE HAKUNA WA KUTUZUIA!

Chukueni hii Leo ni moja ya zile siku Tunasema BAD DAY AT THE OFFICE hakuna kinachoweza kwenda sawa siku ya hivyo ikikutokea!

©️Mdidi kama Mdidi the Writer😎

Sambaza....