Blog

Samatta kukutana na Slavia Prague, ligi ya Uropa.

Sambaza....

Klabu ya soka ya KRC Genk anayocheza mtanzania Mbwana Ally Samatta imepangwa kucheza na Slavia Prague ya Jamhuri ya Cheki katika hatua ya 32 ya michuano ya Europa Ligi.

Genk ambayo ilimaliza kinara wa kundi I ambalo lilikuwa na timu ngumu kama Malmo na Beskitas imepangwa kukutana na miamba hiyo ya Cheki ambao wao walimaliza nafasi ya pili nyuma ya Zenit St. Petersburg katika kundi C.

Genk wataanzia Ugenini katika uwanja wa Eden Arena kabla ya kurudiana baadae kwenye uwanja wa nyumbani wa Genk Cristal Arena.

Samatta mpaka sasa ana mabao matatu katika dakika 426 alizocheza pamoja na kuchangia bao moja katika michuano hiyo ya pili kwa ukubwa kwa ngazi ya vilabu barani Ulaya.

Europa League hatua ya 32 droo

Viktoria Plzen v Dinamo Zagreb

Club Brugge v Red Bull Salzburg

Rapid Vienna v Inter Milan

Slavia Prague v Genk

Krasnodar v Bayer Leverkusen

FC Zurich v Napoli

Malmo v Chelsea

Shakhtar Donetsk v Eintracht Frankfurt

Celtic v Valencia

Rennes v Real Betis

Olympiakos v Dinamo Kiev

Lazio v Sevilla

Fenerbache v Zenit St Petersburg

Sporting Lisbon v Villarreal

Bate Borisov v Arsenal

Galatasaray v Benfica

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x