Mudathir Yahya Abas
Stori

Wababe wa Yanga Sasa Kukipiga Saudi Arabia

Sambaza....

Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) limetangaza kuwa Saudi Arabia itakuwa mwenyeji wa michuano ya CAF Super Cup 2023 kati ya wababe wa Cairo Al Ahly na USM Alger.

Al Ahly, mabingwa wa CAF Champions League, watachuana na washindi wa CAF Confederation Cup USM Alger katika 2023 CAF Super Cup.

 

Mechi hiyo imepangwa kufanyika katika Uwanja wa King Fahd mjini Taif, Saudi Arabia, Septemba 15, kama ilivyoelezwa na CAF kwenye tovuti yao rasmi.

Al Ahly sasa watakuwa wakitafuta Kombe lao la tisa la CAF Super Cup katika historia yake, baada ya kulitwaa mara nane, “The Reds” walipoteza kombe hilo mara mbili pekee mwaka wa 1994 na 2015, huku mara ya pili ikikutana na timu ya Algeria, lakini ilikuwa ES Sétif.

USM Algier mabingwa wa Kombe la Shirikisho Afrika msimu 2022/2023

Wakati huo huo, USM Alger ilinyakua Kombe la Shirikisho la CAF kwa mara ya kwanza baada ya kuifunga Young Africans  kwa bao la ugenini. Taji hilo ni taji la kwanza kabisa la USM Alger katika bara na kwa hivyo watashiriki Kombe lao la kwanza la CAF Super Cup.

Kwa msaada wa Kingfoot.

Sambaza....