
Aliyewahi kuwa kocha mkuu wa klabu ya Yanga , Mwinyi Zahera amedai kuwa asilimia kubwa ya mashabiki wa Yanga wanampenda kwa kiasi kikubwa.
Akizungumza na kipindi cha mshikemshike cha Azam TV , Mwinyi Zahera amedai kuwa ukiwauliza mashabiki 100 wa Yanga basi mashabiki 98 wanampenda Mwinyi Zahera.
“Mashabiki wa Yanga wananipenda mpaka kufa. Ukizungumza na mashabiki 100 wa Yanga basi mashabiki 97 au 98 basi wananipenda sana” – alisema Mwinyi Zahera.

Mwinyi Zahera amedai kuwa kuna baadhi ya mashabiki wa Yanga wachache ambao walitumwa ili waje kumtukana yeye.
“Ni mashabiki wachache tu ambao hawanipenda. Ukiangalia kuna mashabiki walitumwa kuja kunitukana lakini baadaye walikuja kuniomba msamaha”-alimalizia Mwinyi Zahera.
You Might Also Like
Wazee wa moja moja waipumulia Simba!
Bai moja bila dhidi ya Mbeya City, dhidi ya Kagera na sasa dhidi ya Mtibwa Sugar
Simba kuishusha Al-Ahly nchini.
Taarifa kutoka kwa klabu ya Simba imeeleza Al-Ahly wamekubali kushirikiana na Simba katika kujenga kituo cha kukuzia vijana cha soka, pia Alhly kuja nchini kucheza mchezo wa Kirafiki na Simbasc.
Madame Simba CEO, toka ofisini njoo huku uone.
Madam CEO toka sasa kwenye Box lako la U Director maana wakati ni huu na SISI WASWAHILI TUNASEMA USIPOUANIKA UTAULA MBICHI