
Ally Ramadhani "Oviedo" akiwa mazoezini katika uwanja wa Bora Kijitonyama.
Klabu ya soka inayomilikiwa na Manispaa ya Kinondoni KMC fc tayari imeitikia kauli ya rais ya kurudisha michezo na tayari wameingia kambini kujiandaa na kumalizia michezo iliyokabi ya Ligi.
Kmc imeanza mazoezi tangu siku ya Jummane tarehe 26 katika uwanja wa Bora Kijitonyama, huku wakiweka kambi yao maeneo ya Makongo Juu karibu na Chuo cha Kikuu cha Ardhi.
Mpaka Ligi inasimama kutokana na ugonjwa wa corona KMC unashika nafasi ya 15 ikiwa na alama 33 huku ikiwa imeshuka dimbani mara 29. Kabla ya Ligi kusimama KMC ilikua katika muendelezo mzuri baada ya kushinda michezo minne mfululizo na hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kujitoa katika eneo hatari la kushuka daraja.
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.