
Marcel Kaheza Boniventure akiwa katika uzi Majimaji fc.
Mshambuliaji wa timu ya Majimaji, Marcel Kaheza amechaguliwa mchezaji bora wa ligi kuu ya Vodacom mwezi Aprili.
Kaheza atapewa fedha milioni moja na wadhamini wakuu wa ligi Kampuni ya Vodacom, kisimbuzi cha Azam TV
Kaheza amewapiku washambuliaji nyota wa timu ya Simba, John Bocco na Emmanuel Okwi kwenye kinyang’anyiro hicho.
Katika mwezi huo Kaheza amefunga mabao saba yakiwemo matatu ‘hat trick’ katika mchezo mmoja.
dhidi ya Ruvu Shooting vile vile ameiwezesha Majimaji kutoka mkiani mwa msimamo mwezi Machi hadi nafasi ya 14 sasa.
Katika mwezi uliopita Emmanuel Okwi alifunga magoli 3 na kutoa pasi za mwisho 2 wakati John Bocco akifunga magoli manne (4) na kutoa pasi mbili za mwisho za magoli.
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.