Blog

Timu ya Taifa yafuzu Afcon Misri!

Sambaza....

 

Timu ya Taifa ya Soka la Ufukweni ya Tanzania imefuzu kucheza Fainali za Africa zitakazofanyika nchini Misri.

Timu ya Tanzania imefuzu kucheza Fainali hizo baada ya mpinzani wake Afrika Kusini kuwasilisha barua ya kujiondoa katika mashindano.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) tayari wametujulisha taarifa hiyo ya kufuzu kucheza Fainali hizo za Afrika zitakaofanyika Misri mwaka huu kuanzia Desemba 9-Desemba 14,2018 na kushirikisha nchi Nane.

Timu ya Taifa ya Tanzania ya Soka la Ufukweni ilikuwa kambini kujiandaa na mchezo huo uliokuwa uchezwe Jumapili Septemba 9,2018.

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x