
Timu ya soka inayomilikiwa na jeshi la Kujenga Taifa JKT Tanzania imeendeleza kugawa vipigo katika michezo inayopigwa katika uwanja wao wa nyumbani baada ya leo kuiadhibu African Lyon ya Dar es salaam.
Katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Generali Isamunyo bao lá Abdulrahmani Mussa katika dakika ya 50 lilitoshakuwapa alama tatu vijana wa Bakari Shime waliokua wenyeji.
Lyon ikiongozwa na washambuliaji wao Victor da Costa na Haruna Moshi “Boban” hawakuweza kabisa kufurukuta mbele ya walinzi wa JKT Tanzania wakiongozwa na Mohamed Fakhi na Maiko Aidan.
JKT Tanzania sasa wanasubiri kuwakaribisha Allience fc katika dimba lao la nyumbani mchezo utakaopigwa Jumamosi hii tarehe 6 October!
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.