Bila shaka dhambi inayoongoza ndani ya dimba la kandanda ni uongo. Ni kawaida mchezaji kuunawa mpira na akambishia refa kuwa hajashika. Kujiangusha kwenye box la 18 ili wapate penalty na danganya toto nyingine nyingi.Watu wa mpira wanalijua hili, haiitaji maelezo meengi!
Ni nadra sana kwa mchezaji wa mpira kukubali makosa, atabisha tu!
Ok! Turudi mwaka 2012 katika mechi ya ligi kuu ya Italia ya Serie A kati ya Napoli na Lazio. Miloslov Klose alifunga goli akiunganisha mpira wa kona.
Wakati wachezaji wenzake wa Lazio wakiendelea kushangilia, Klose alimfuata refa na kumwambia aliupiga mpira kwa mkono na kufunga.
Refa alibadili maamuzi ndipo wachezaji wa Napoli walimfuata Klose kumpongeza na kumshukuru kwa kuwa mkweli na muungwana.
Unaweza soma hizi pia..
Unakumbuka Kali ya Zidane Pale Ujerumani?
Zinedine Zidane Yazid maarufu kama Zizzou alikuwa na kiwango bora kwenye michuano hiyo ya kombe la Dunia 2006
Jinsi Simba Walivyopeleka Maafa Zambia Mwaka 1979
Magazeti ya Zambia yakiandika kuhusu mechi hiyo waliita kuwa "mechi ya matokeo mabaya kabisa kuwahi kutokea kwa Wanderers katika historia" na kwamba ni "Jambo kubwa kabisa katika sikukuu ya wajinga duniani
Yanga yatwaa ubingwa, Kizota mfungaji bora.
Yanga ambao wengi hawakuipa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa baada ya kuanza vibaya michuano hiyo kwa kuchapwa mabao 3-1 kwenye mchezo wao wa kwanza
Unaikumbuka hii Pamba Sc!?
Tuambie unaikimbuka kwa lipi Pamba hii ambayo ilikua mwiba katika miaka ya tisini haswa katika Dimba la CCM Kirumba pale Mwanza!?