Bila shaka dhambi inayoongoza ndani ya dimba la kandanda ni uongo. Ni kawaida mchezaji kuunawa mpira na akambishia refa kuwa hajashika. Kujiangusha kwenye box la 18 ili wapate penalty na danganya toto nyingine nyingi.Watu wa mpira wanalijua hili, haiitaji maelezo meengi!
Ni nadra sana kwa mchezaji wa mpira kukubali makosa, atabisha tu!
Ok! Turudi mwaka 2012 katika mechi ya ligi kuu ya Italia ya Serie A kati ya Napoli na Lazio. Miloslov Klose alifunga goli akiunganisha mpira wa kona.
Wakati wachezaji wenzake wa Lazio wakiendelea kushangilia, Klose alimfuata refa na kumwambia aliupiga mpira kwa mkono na kufunga.
Refa alibadili maamuzi ndipo wachezaji wa Napoli walimfuata Klose kumpongeza na kumshukuru kwa kuwa mkweli na muungwana.

Unaweza soma hizi pia..
Kituko cha Oliver Khan na kufungwa kwa Bayern.
Golikipa Oliver Kahn alipanda kwenda kushambulia, ilipopigwa kona aliruka juu na kuupiga mpira kwa mikono na ukatinga ndani ya nyavu
Goli la dhahabu na kifo kilichoandaliwa kwa Wataliano!
Naweza kusema angalau sasa zama zimebadilika kwa kiwango kikubwa, lakini zamani kidogo ukicheza na mwenyeji basi jiandae kupita njia ya mateso ya Golgotha
Laana ya kocha wa Benfica na kombe la Ulaya!
Benfica haitakuja kuchukua ubingwa wowote wa Ulaya mpaka ipite miaka 100.
Di Canio mtukutu mwenye tuzo ya Fairplay!
Zikiwa zimesalia dakika tano matokeo yakiwa ni 1-1 huku West Ham wakihitaji point tatu muhimu, wana London wengi hawakumuelewa Di Canio akiwepo kocha wake Harry Redknapp