Blog

Nonga apewa mtaa.

Sambaza....

Wakazi wa mji wa Shinyanga pale Ngokolo wamempa heshima ya kipekee mshambuliaji wa Lipuli Fc, Paul Nonga, kwa kuupa mtaa jina lake.

Nonga ameimbia Kandanda.co.tz kuwa heshima hii aliyopewa ya mtaa wake alipozaliwa kupewa jina lake ni heshima kubwa kwake na anadeni kubwa sana la kulipa. Alizingumza nasi wakati akiwa safarini kuelekea Musoma kwaajili ya mchezo wa Ligi kuu dhidi ya Biashara United.

Sasa kibao kimoja cha mtaa huo kineandikwa Nonga Street.

Nonga amewahi kuzichezea kwa mafanikio klabu za Mwadui, Mbeya City na Yanga Sc kabla ya kujiunga na klabu ya Lipuli FC ambayo ipo nafasi za juu ligi kuu pamoja na kuingia nusu fainali ya kombe la shirikisho Tanzania

Sambaza....
Subscribe
Notify of

0 Maoni
Inline Feedbacks
Tazama Maoni Yote
0
Tungependa kupata maoni yako, tafadhali tuambiax
()
x