
Moja ya mikutano ambavyo timu inaweza kutangaza viingilio au utaratibu wa mapato yao. Pichani ni Haji Manara, Msemaji wa Simba SC.
Kuelekea mechi ya watani wa jadi kati ya Simba na Yanga tambo zinazidi kuwa nyingi ambapo Leo msemaji mkuu wa Simba amedai kuwa mashabiki wa Yanga wanapokutana akili zinakuwa moja.
“Wewe mchukue profesa yoyote wa chuo kikuu, mchukue profesa ambaye ni daktari bingwa ambaye ni shabiki wa Yanga afu waweke pamoja na shabiki wa Yanga ambaye ni muuza ubuyu , akili zao zinakuwa pamoja”
“Hata baba yangu huwa namuuliza, kuna wakati nikiwa nazungumza na baba yangu kwenye mambo mengine anaonekana ni Genius kweli, lakini linapokuja suala la Yanga U-genius wake unapotea”- alimalizia kwa kusema hivo , msemaji huyo alikuwa anahojiwa na kituo cha radio cha Wasafi Fm
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.