
Kuelekea mchezo namba 260 wa Ligi Kuu Bara ambao Yanga atakua mwenyeji wa Simba katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam tayari shirikisho la miguu nchini limetaja waamuzi watakaoamua mchezo huo.
TFF leo wamewataja waamuzi hao kutoka mikoa ya Morogoro, Tanga, Singida na Dar es salaam. Huku wengi wao wakiwa ni waamuzi wazoefu wakiwa wameshashiriki katika kuchezesha michezo hiyo ya Simba na Yanga.
Mwamuzi wa kati ni Martin Saanya (Morogoro), mwamuzi msaidizi namba moja ni Mohamed Mkono (Tanga), mwamuzi msaidizi namba mbili ni Frank Komba (Dar es salaam) na mwamuzi wa akiba ni Elly Sassii wa Dar es salaam.
Pia waamuzi wa ziada watakua ni Abdallah Mwinyimkuu (Singida) na Ramma Kayoyo (Dar es salaam) na mechi kamishina Mohamed Mkweche.
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.