Sven Vandebroek na Selemani Matola
Ligi Kuu

Kocha Simba awaita mashabiki Mbeya!

Sambaza....

Kocha Msaidizi, Suleiman Matola amewataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi katika mechi mbili ndani ya Jiji la Mbeya huku akiwahakikishia furaha kwani ana uhakika wa kupata ushindi.

Kikosi cha Simba kesho kitashuka katika Uwanja wa Sokoine kuikabili Mbeya City na Jumapili kitarejea dimbani hapo kumenyana na Tanzania Prisons ambayo katika mchezo wa kwanza uliopigwa jijini sare uliisha kwa suluhu.

Mashabiki wakifwatilia mchezo wa timu yao katika uwanja wa Taifa.

Matola amesema hali ya hewa ya jiji la Mbeya ni baridi kali lakini wachezaji wapo kwenye hali nzuri na wana ari kitu kinachomfanya kuamini katika kupata ushindi kwenye mechi hizo mbili.

Kiungo huyo wa zamani wa Simba amesisitiza mashabiki kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kutoa sapoti kwa wachezaji.

“Hali ya hewa ya Mbeya ni baridi sana, tumeanza mazoezi tangu jana kwa awamu moja, wachezaji wako vizuri tayari kwa mapambano.

Tunawaomba Wanasimba watusapoti kwa kujitokeza kwa wingi uwanjani tunachowaahidi ni kuwa hatutawaangusha kutokana na jinsi wachezaji walivyo tutahakikisha lazima tupate matokeo ya ushindi tukianza na mchezo wa kesho dhidi ya City,” amesema Selemani  Matola alipokua akiongea na touvti ya klabu.

Sambaza....