
Harrison Mwakyembe waziri mwenye dhamana ya michezo!
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr. Harrison Mwakyembe amezungumaza na kituo cha redio cha Efm katika kipindi cha michezo na kuweka wazi jinsi alivyomuulizia nyota wa DR Congo David Molinga.
Katika mchezo uliowakutanisha JKT Tanzania dhidi ya Yanga katika dimba la Jamuhuri Dodoma Jumatano June 17 ambapo matokeo yalikua sare kwa bao moja kwa moja, Mh. Mwakyembe alikuepo uwanjani hapo kuushuhudia.

Mwakyembe amesema:”Unajua timu za jeshi hazina mapumziko, wao kipindi cha Corona hakuna Corona lazima wawe fiti kwa kufanya mazoezi sasa nilishangaa nilipoona kikosi cha Yanga hakina Molinga.
“Niliwauliza wale ambao nilikuwa nao, jamani mbona Molinga hapa simuoni akianza ila baadaye kidogo nilimuona akiingia, wale ni wanajeshi lazima kikosi kitakachopambana nao kiwe na nguvu muda wote.”

Katika mchezo huo JKT ndio waliokuwa wakwanza kupata bao kupitia kwa Michael Aidan kabla ya Patrick Sibomana kusawazisha kipindi cha pili. Pia ilishuhudiwa vurugu kubwa mchezo ulipokua unaelekea mwishoni na kupelekea Mwinyi Kazimoto na Lamine Moro kuonyeshwa kadi nyekundu.
Unaweza soma hizi pia..
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.
Kola na mfupa uliomshinda Mayele!
Licha ya Fiston Mayele kusifiwa na kuoneoana ni moja ya washambuliaji hatari katika Ligi lakini hakufanikiwa kufunga
George Mpole anaishi ndoto zetu!
juhudi binafsi za George Mpole na ndio maana utofauti wa mabao ya kufunga na kufungwa ni 1 kwao lakini yeye pekeake Mpole ana mabao 13.