
Yikpe
Muhamasishaji mpya wa Yanga Mheshimiwa Jerry Muro ambae ni mkuu wa wilaya ya Arumeru leo ameongea na timu ya Wananchi Yanga kupitia redio ya Wasafi fm.
Katika mahojiano hayo Murro ameonekana kulalamikia ubora wa kikosi cha Yanga haswa wachezaji wa kigeni huku akiwatajaa baadhi yao kama Molinga na Yikpe.

Jerry Murro” Huyu Yikpe tuongee ukweli hastahili hata kucheza Ligi daraja la pili, hana uwezo wa kucheza Yanga kabisa. Ukiangalia yeye ni mrefu sawa na John Bocco lakini hana vitu ambavyo Bocco anavyo, hana cha chenga wala kugeuka.
Ni afadhali ya Mrisho Ngassa, huyu “uncle” atatusaidia Yanga kuliko Yikpe hana msaada yoyote na Yanga.”
Unaweza soma hizi pia..
Rafiki yangu Ajib ananipa unyonge!
Ajib hajui mpira? Hapana. Kuna timu haitamani kipaji cha Ajib? Hapana. Katika ubora wake kuna timu katika ligi yetu Ajib anaweza kukaa benchi?
Juma Mgunda na utamu wa Coastal Union yake!
Mgunda mpaka sasa ameiongoza Coastal Union katika michezo 10 ya Ligi.
Alli Kamwe: Lengo Yanga na sio Mayele!
Mayele ni mchezaji muhimu kwenye Timu. Yanga inamuhitaji zaidi akiwa Fiti uwanjani kuliko yeye anavyokihitaji kiatu cha Ufungaji bora kabatini kwake.
Msemaji Simba: Mambo ni magumu!
Kila mwanasimba anatakiwa kufahamu hilo na kukubali mambo ni magumu.