
KOCHA Mkuu wa Yanga, Luc Eymael, amesema kuwa anamtazama kwa ukaribu beki wa zamani wa timu hiyo, Abadlah Shaibu ‘Ninja’ ili kuona kama anaweza kufiti kwenye mfumo wake kabla ya kuruhusu asaini dili ndani ya klabu hiyo.
Ninja alikitumikia kikosi cha Yanga msimu wa 2018/19 kabla ya kuondoka na kutua MFK Vyskov inayoshiriki Ligi Daraja la Tatu nchini Jamhuri ya Czech.Baada ya kujiunga na klabu hiyo, alitolewa kwa mkopo kwenda LA Galaxy ya Marekani kabla ya kurejea kwenye timu yake ya zamani.
Kwa sasa Ninja yupo Tanzania akifanya mazoezi na Yanga. Eymael alisema: “Shaibu kwa sasa sio mchezaji wa Yanga ila amekuja kwa ajili ya kufanya majaribio, ninamtazama ili kuona akikidhi vigezo basi tutamalizana naye.”
Unaweza soma hizi pia..
Mbinu mpya za Yanga zilizoacha lawama kwa kipa wa Dodoma Jiji
Nasredeen Nabi ilimlazimu kutoka katika mfumo wake wa siku zote wa kumtegemea Fiston Mayele na kubadili mbinu ili kupata ushindi.
Simba na Yanga kukutana tena mwezi huu.
Ratiba ya kombe la Azamsports Federation Cup imetolewa leo na Shirikisho la Soka nchini TFF huku pia wakitaja na viwanja vitakavyotumika katika michezo hiyo ya nusu fainali.
Kipa Dodoma katolewa tuu kafara!
Ndani ya miaka miwili unataka kuniambia ameisha kabisa? Je hatupaswi kumshukia kocha wake wa makipa?
Alli Kamwe: Yanga imeifunga Yanga B!
Bao la 2 la Yanga ni OFFSIDE. Kama Shuti la Mauya lingekwenda moja kwa moja, hakuna tatizo.